KATIBA YA VIWAWA: 2010
YALIYOMO
i
Vifupisho
ii
Utangulizi
- Maana ya Viwawa
- Anwani
ya Chama
- Ofisi ya chama
- Dira
ya Viwawa
- Utume
wa Viwawa
- Malengo
ya Viwawa
- Uanachama
- Muundo wa Chama
- Uongozi wa Chama
- Mikutano
- Wajumbe wa Mikutano ya Viwawa
- Majukumu ya Kamati
- Mapato ya chama
- Kamati ndogondogo
- Muhimu
- Mengineyo
i. TAFSIRI YA VIFUPISHO
o KAMATI - Kamati Tendaji
o VIWAWA - Vijana Wakatoliki Wafanyakazi
o TYCW -
Tanzania Young Catholic workers.
o TEC - Tanzania
Episcopal Conference.
o ICYCW – International Coordination of Young
Christian Workers.
o YCS – Young
Catholic Students
o OFM – Ordo
Fratrum Minorum
ii. UTANGULIZI
HISTORIA YA VIWAWA TANZANIA :
VIWAWA ilianzishwa mwaka 1924 mji wa Brussel
nchini Ubelgiji na Kadinali Joseph
Cardjin nakupitishwa rasmi kama Chama
cha Kitume cha Vijana Kimataifa na Baraza la Kipapa Vatcan mwaka 1950.Kadinali
Joseph Cardjin pia alianzisha YCS,hivyo VIWAWA na YCS alianzisha yeye.
Makao Makuu ya Viwawa Duniani Yako
Roma – Italia.
Viwawa iliingia Tanzania mwaka 1959
katika Parokia ya Msimbazi, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, chini ya Mwanzilishi
Pd. Lucas Gaemperle OFM, badaye mwaka
1960 alifika nchini kwetu Pd. Hendrikus Johannes Brinkhof maarufu kama Pd
Mansuetus ambaye alimsaidia kwa karibu sana, padri Lucas kuueneza utume wa
viwawa nchini kwetu, na kufuatiwa na Parokia ya
St. Joseph, Kurasini, Magomeni, Chang’ombe, Kibaha.
Mwanzilishi wa viwawa duniani
Kardinali Joseph Cardijn alitembelea Tanzania ,
jimbo la Dar es salaam
tarehe 17 – 6 – 1960.
Padri Lucas Gaemperle OFM ambaye alikuwa mwanzilishi wake
alitembea sehemu nyingi za Afrika na Ulaya kwa lengo la kujifunza utume huu. Mwaka 1961 VIWAWA Tanzania walitembelewa na mjumbe
kutoka Makao Makuu Roma Italia na alitembelea matawi ya Dar es Salaam na Moshi. Mjumbe huyo alifanyakazi ya kuunganisha utume
huu hapa Tanzania na huko Zambia . Mwezi Novemba 1964 Kamati kuu ya VIWAWA
ulimwenguni walifanya mkutano hapa Tanzania ,
Mkutano huu ulifuatiwa na ziara za mafunzo ili kuona maendeleo ya Viwawa hapa Tanzania .
Mnamo mwaka 1966 Viwawa walifanya
mkutano mkuu wa kitaifa na ni majimbo mawili tu ndiyo yalihudhuria Dar es Salaam na Moshi
yakiwakilishwa na wajumbe kumi na mmoja.
Mwaka 1973 mkutano mkuu ulifanyika jimboni Iringa na ndipo kwa mara ya
kwanza katiba ya Viwawa iliundwa, na kupitishwa rasmi kama
chama cha kitume cha vijana na Baraza la Maaskofu katoliki Tanzania (TEC) mwaka
1979. Mshauri wa kwanza wa viwawa Taifa Padri Pius Shayo aliyeteuliwa katika
mkutano mkuu wa baraza la maaskofu Tanzania uliofanyika tarehe 23 – 27
October, 1979.
Baada ya kupitishwa hapo
kilitambulika pote Tanzania kama Chama cha Vijana Wakatoliki Wafanyakazi Tanzania
(VIWAWA)Mpaka sasa, chama hiki kipo majimboni, kuanzia ngazi ya Jumuiya, Mtaa,
Kanda, Kigango, Parokia, Jimbo, Taifa na Kimataifa.
![]() |
1.0 MAANA YA VIWAWA
1.1 VIWAWA ni chama cha
kitume cha Vijana Wakatoliki Wafanyakazi ambao wanatumwa na Kanisa ili kueneza
habari njema ya kwamba Yesu Kristu ndiye njia ya ukweli na uzima kwa vijana
wote katika maisha yao ya kila siku.
1.2 Wafanyakazi: Ni vijana wa wanaume na wanawake waishio
mijini, vijijini na walio kwenye masomo, mafunzo ya fani mbalimbali, walio katika ajira rasmi na zisizo rasmi.
1.3 Viwawa ni chama ambacho
kinawaunganisha vijana na kuwasaidia waone hali yao, kuamua juu yake katika
mwanga wa Injili na kuwaongoza kufanya matendo ya kubadilisha hali zao na
kutengeneza ziwe nzuri zaidi kwa njia ya Tafakari ya Maisha.
Chama hiki huongozwa na vijana
wenyewe katika ngazi zote na huwa na Mshauri na Mlezi kwa ngazi ya
Parokia,Jimbo na Taifa.
2.0 ANWANI YA CHAMA:
Vijana Wakatoliki Wafanyakazi.
S.L.P 2133,
DAR ES SALAAM - TANZANIA.
Barua pepe: viwawatycw@yahoo.com
3.0 OFISI ZA
VIWAWA.
3.1 Ofisi ya viwawa taifa
itakua pale yalipo makao makuu ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.(TEC)
3.2 Ofisi ya jimbo itakua
pale yalipo makao Makuu ya Jimbo.
3.3 Ofisi ya parokia itakua
parokiani.
4.0 DIRA YA
VIWAWA
Kumwona Kijana Mkatoliki Mfanyakazi anayejimudu katika
maisha yake ya kimwili na kiroho kwa kutumia njia ya Tafakari ya Maisha.
5.0 UTUME WA
VIWAWA
Kumwezesha kijana kuwa Mkristo wa kweli ambaye ana ujasiri
wa kurekibisha,
kuendeleza na kudumisha taratibu
za utamaduni, uchumi, siasa na
utaalamu kufuatana na mpango wa
Mungu.
6.0 MALENGO YA
VIWAWA
6.1 Kuwawezesha Vijana kutambua wajibu wao katika
kujielimisha na kujitegemea katika maisha yao .
6.2
Kustawisha na
kusaidia Kanisa kwa kushiriki katika kazi za Kanisa, kuhusu maendeleo ya
Kiroho, Kimwili, Kiakili na Kijamii.
6.3 Kutangaza habari za Kanisa na kujaribu kwa kila hali
kuleta uhusiano mwema baina ya vyama vya kitume,madhehebu mbalimbali na dini
nyingine.
6.4 Kuchukua hatua za kufaa kuendeleza mambo yote
yanayoonekana kwamba ni ya manufaa kwa Kanisa na Ustawi wa jamii.
6.5 Kuwajenga vijana katika mazingira ya kuwa na mwenendo
mwema kwa kanuni ya Tafakari ya Maisha inayoongozwa na mtindo wa Kuona-Kuamua na
Kutenda. Na mitindo mingine ya malezi inayofaa.
6.6 Kuwakumbusha
vijana wote kwamba sote tunategemeana kwa kushauriana, kuongozana na
kufundishana kimwili na kiroho.
7.0 UANACHAMA:
Kuna aina tatu za uanachama.
7.1 Wanachama
washiriki
7.1.1
Awe kijana Mkatoliki
mwenye umri kati ya miaka 14 hadi 17.
7.2 Wanachama
kamili
7.2.1
Kijana
Mkatoliki mwenye Ubatizo.
7.2.2
Awe na umri kati
ya miaka 18 hadi 35.
7.2.3
Awe mwenye Akili
timamu.
7.2.4
Awe na Mapenzi na VIWAWA..
7.2.5
Vijana
ambao wameowa na kuolewa pia wanaweza kuwa wanachama na viongozi.
7.3
Wanachama maalumu
7.3.1
Aliyekwisha kuwa
mwanachama kamili.
7.3.2
Watu wa wazima wenye mapenzi mema na chama.
7.4 Wajibu wa
Mwanachama.
7.4.1
Kukubali
kuongozwa na Mwongozo wa chama na kutekeleza malengo yake.
7.4.2
Kushiriki mikutano
ya chama kwa mujibu wa KATIBA.
7.4.3
Kushiriki
shughuli zote za VIWAWA.
7.4.4
Kushiriki katika
chaguzi mbalimbali za VIWAWA.
7.4.5
Kulipa ada na michango maalum kwa wakati unaotakiwa.
7.4.6
Kuunga mkono na kusaidia kwa vitendo maendeleo ya VIWAWA.
7.4.7 Kusikiliza na kufuata maelekezo mbalimbali
ya Uongozi.
7.5 Haki za
Mwanachama
7.5.1
Anahaki ya
kuchagua au kuchaguliwa kwa mujibu wa ibara namba (7.1,2) na (9.2).
7.5.2
Kuchangia hoja na
kusikilizwa katika mikutano kwa nidhamu
7.5.3
Kushiriki
shughuli zote za VIWAWA kwa mujibu wa KATIBA.
7.5.4
Anahaki ya kupata
huduma, faida zitokanazo na chama kwa mujibu wa taratibu za chama mahalia.
7.5.5
Mwanachama
maalumu hawezi kuchagua au kuchaguliwa katika Uongozi.
7.5.6
Mwanachama
maalumu hawezi kufanya maamuzi kwa niaba ya Kamati Tendaji
7.5.7
Mwanachama
anapotuhumiwa anahaki ya kupewa fursa za kujieleza,kujitetea.
7.6 Ukomo wa
Uanachama
7.6.1
Akikiuka maadili
ya chama kama kushiriki katika kuihujumu
VIWAWA
7.6.2
Kufariki dunia.
7.6.3
Kuvuka kikomo cha umri wa miaka 35.
7.6.4
Hiari ya mwanachama ambayo itadhibitishwa na Uongozi.
8.0 MUUNDO WA CHAMA.
Kutakuwa
na Ngazi Sita zaViwawa
8.1 Ngazi ya Jumuiya Ndogondogo
8.2
Ngazi ya Kigango,Kanda.
8.3 Ngazi ya Parokia.
8.4 Ngazi ya Jimbo.
8.5 Ngazi ya Taifa.
8.6 Ngazi ya Kimataifa.
9.0 UONGOZI WA CHAMA.
9.1
Ngazi za uongozi
9.1.1
Mwenyekiti
9.1.2
Makamu wa Mwenyekiti
9.1.3
Katibu
9.1.4
Katibu Msaidizi
9.1.5
Mhazini
9.1.6
Mhazini Msaidizi
9.1.7
Mratibu (ngazi ya Jimbo na Taifa)
9.1.8
Wajumbe wa
kuteuliwa wasio zidi wa tatu.
9.1.9
Mshauri
9.2 Sifa za
uongozi
9.2.1
Kijana Mkatoliki
9.2.2
Asiwe na kizuizi
chochote cha Sakramenti.
9.2.3
Mwenye umri kuanzia miaka 18 hadi 35.
9.2.4
Awe na Akili
timamu
9.2.5
Uwezo na kipaji cha kuongoza, busara na hekima.
9.2.6
Awe na mapenzi na
Viwawa
9.2.7
Kwa nafasi ya
katibu awe na uwezo wa kusoma na kuandika vizuri.
9.2.8
Kwa nafasi ya
Mhazini awe Mwaminifu, na kwa ngazi ya Parokia, Jimbo na Taifa awe na Ujuzi au
Uzoefu wa maswala ya Fedha.
9.2.9
Kiongozi katika
ngazi ya Jimbo na Taifa lazima awe na sifa za ziada kama
uzoefu wa uongozi walau mwaka mmoja na kiwango cha elimu walau kidato cha nne
au elimu inayolingana na hiyo.
9.3 Uchaguzi wa
Viongozi
9.3.1
Viongozi watachaguliwa na mkutano mkuu baada ya miaka
mitatu.
9.3.2
Kiongozi anaweza kuchaguliwa vipindi vitatu mfululizo
kama ataonekana anafaa.
9.3.3
Uchaguzi utafuata taratibu zote za uchaguzi kama
zilivyoainishwa kwenye katiba ya
Halmashauri ya Walei.
9.3.4
Wajumbe watakaoruhusiwa kupiga au kupigiwa kura ngazi ya
taifa ni viongozi wa ngazi ya jimbo, kwa ngazi ya jimbo ni viongozi wa parokia,
na kwa ngazi ya parokia ni viongozi wa kigango,kanda au jumuiya.
9.3.5
Viongozi wa Kamati Tendaji iliyomaliza muda wake ni wajumbe halali wa kupiga na kupigiwa kura
kwa kuzingatia ibara namba (7.2).
9.3.6
Mjumbe asiyekuwepo katika kikao cha uchaguzi kwa udhuru
anaweza kuchaguliwa kama anasifa toshelezi za kiongozi.
9.3.7
Viongozi wakuu watatu watoke karibu na ofisi ya ngazi
husika ili kuleta ufanisi wa kazi za Utume hasa kwa nafasi ya Mhazini.
9.3.8
Uchaguzi ngazi ya jumuiya, kanda, kigango utasimamiwa na
viongozi wa viwawa ngazi ya parokia. Uchaguzi ngazi ya parokia utasimamiwa na
viongozi wa viwawa jimbo husika, ngazi ya jimbo utasimamiwa na viongozi Viwawa
ngazi ya Taifa ngazi ya Taifa utasimamiwa na Idara ya Walei TEC.
9.4 Upigaji Kura
9.4.1 Kura zote ni lazima zifanyike kwa njia ya
siri, kiongozi anayechaguliwa lazima apate zaidi ya nusu ya kura zote. Kama
zikilingana mara mbili Msimamizi wa uchaguzi atakuwa na uwamuzi wa mwisho.Viongozi
wapya watadhibitishwa na Uongozi wa Kanisa ngazi husika.
9.5 Mshauri,Mlezi wa chama
9.5.1 Mshauri
wa Taifa atateuliwa na Baraza la Maaskofu
9.5.2 Mshauri
wa Jimbo atateuliwa na Mkuu wa Jimbo
9.5.3
Mshauri wa Parokia
atateuliwa na Paroko.
9.6
Wajibu wa Mwenyekiti na
Makamu Mwenyekiti
9.6.1
Atakuwa kiongozi na Msemaji Mkuu wa VIWAWA.
9.6.2
Atasimamia mikutano ya kamati tendaji na mikutano ya VIWAWA.
9.6.3
Asaidie na kuangalia kwamba viongozi wengine wote
wanafanyakazi zao ipasavyo.
9.6.4
Kuona kuwa kila mjumbe anapata nafasi ya kutoa maoni yake
katika mikutano.
9.6.5
Agawanye kazi na madaraka mengine kwa viongozi wenzake wa
kamati ili asifanye kazi peke yake.
9.6.6
Atakuwa na kura ya uamuzi endapo kutatokea sare katika
kura.
9.6.7
Atawajibika kwa
kamati tendaji.
9.7 Wajibu wa
Katibu na Katibu Msaidizi
9.7.1
Atakuwa Mtendaji wa VIWAWA.
9.7.2
Atatunza kumbukumbu zote za Mikutano.
9.7.3
Ataandaa agenda na dondoo za vikao
9.7.4
Atatoa taarifa zote kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka kuhusu
maendeleo ya chama, katika kipindi kilichopita.
9.7.5
Kutayarisha na kuitisha mikutano yote ya chama
akishauriana na Mwenyekiti.
9.7.6
Kupokea na kuzishughulikia ipasavyo barua zote zinazohusu
Chama.
9.7.7
Atawajibika kwa kamati tendaji
9.8
Wajibu wa Mhazini na
Mhazini Msaidizi
9.8.1
Kutunza fedha za chama sehemu salama Benki. Pia kuona
kuwa zinatumiwa kwa njia inayofaa.
9.8.2
Kuweka vitabu vya fedha kwa uangalifu.
9.8.3
Atatoa taarifa zote za fedha kwenye mikutano yote halali
ya chama.
9.8.4
Kutayarisha makisio ya mapato na Matumiza ya fedha za
Chama na kuwasilisha mbele ya kamati ya utekelezaji ili yathibitishwe.
9.8.5
Atatoa kumbukumbu zote za fedha kila itakapohitajika.
9.8.6
Kuhimiza na kupanga njia za kupata fedha za chama na
kuona kwamba malipo yanafanywa kwa kadiri ya mapato na matumizi yaliyokubaliwa
na chama – akishirikiana na Kamati Tendaji.
9.8.7
Atawajibika kwa
kamati tendaji
9.9 Wajibu wa
Mshauri,Mlezi
9.9.1
Kutoa mashauri ya Kiroho na ya shughuli za maendeleo
katika chama.
9.9.2
Kuhudhuria
Mikutano yote ya chama
9.9.3
Kuwa Mjumbe wa hadhi bila kuwa na kura.
9.9.4
Kudumisha na uhusiano mwema kati ya viongozi na wanachama
kwa ujumla.
9.10 Kuacha au
Kuachishwa Uongozi
9.10.1
Kushindwa kuhudhuria
mikutano mitatu mfululizo bila taarifa maalum.
9.10.2
Kukiuka maadili
ya uongozi.
9.10.3
Kwa kutoa taarifa
ya maandishi kwa viongozi waliopo mwezi mmoja kabla.
9.10.4
Kutokana na
sababu zisizo epukika.
9.10.5
Iwapo Kiongozi wa
ngazi ya chini atateuliwa au kuchaguliwa kushika Nafasi ya ngazi ya juu ya
Viwawa katika nafasi ileile Atajiuzulu na Atabaki kuwa mjumbe wa Kamati Tendaji
wa ngazi ile aliyojiuzulu.
9.10.6
Nafasi iliyoachwa
wazi kwa sababu yoyote ile, kiongozi wa muda atateuliwa na Kamati Tendaji
kushika madaraka mpaka uchaguzi mwingine.
9.10.7
Ikiwa zaidi ya
nusu viongozi wamejiuzulu uchaguzi utaitishwa upya kwa nafasi zote.
10.0
MIKUTANO
Kutakuwa
na Mikutano ifuatayo ya VIWAWA
10.1
Kamati ya Utendaji
10.1.1 Kamati Tendaji ngazi ya Taifa,itakutana kila baada ya
miezi mitatu (mara nne kwa mwaka). Ngazi ya Jimbo kila baada ya miezi miwili
(mara sita kwa mwaka) ngazi ya parokia,kigango na kanda mara moja kwa mwezi.
10.1.2 Kikao cha dharura cha Kamati tendaji kinaweza
kuitishwa endapo kuna haja na ulazima wa kufanya hivyo.
10.1.3 Kikao cha Kamati Tendaji kitaitishwa na Katibu kwa
kushauriana na Mwenyekiti.
10.1.4 Wajumbe wasiopungua nusu ya wajumbe wote wa Kamati ya
Utendaji wanaweza kuitisha kikao kwa maandishi.
10.1.5 Taarifa ya kikao cha Kamati Tendaji itatolewa kwa wajumbe siyo chini ya
siku kumi kabla ya kikao.
10.1.6 Endapo idadi ya wajumbe waliohudhuria haifikii nusu ya
wajumbe wa Mkutano, mkutano utahairishwa.
10.2
Halmashauri ya Utekelezaji
10.2.1 Itakutana mara moja kwa mwaka Taifa, Jimbo mara tatu,
Parokia mara nne.
10.2.2 Kuitisha Kikao cha dharura cha Halmashauri endapo kuna
haja na ulazima wa kufanya hivyo.
10.2.3 Kikao cha Halmashauri kitaitishwa na Katibu kwa
kushauriana na Mwenyekiti...
10.2.4 Wajumbe wasiopungua theluthi moja ya wajumbe wote wa
Halmashauri wenye haki ya kuhudhuria wanaweza kuomba kimaandishi kuitishwa kwa
kikao cha Halmashauri.
10.2.5 Taarifa za kikao cha Halmashauri itatolewa kwa wajumbe
siyo chini ya siku thelathini kabla ya kikao.
10.2.6 Endapo idadi ya wajumbe waliohudhuria haifikii nusu ya
wajumbe wa Mkutano, mkutano utahairishwa kwa muda usiopungua miezi miwili.
Lakini endapo mahudhurio ya wajumbe hao ni zaidi ya theluthi moja ya idadi ya
wajumbe wote wa Mkutano basi mkutano utafanyika.
10.3
Mkutano Mkuu
10.3.1 Ndicho kikao cha juu kuliko vyote vya VIWAWA. Utaitishwa mara moja kwa mwaka Taifa, Jimbo mara mbili,
Parokia mara tatu. Kigango na kanda mara
nne.
10.3.2 Mkutano Mkuu wa dharura utaitishwa endapo kuna haja na
ulazima wa kufanya hivyo.
10.3.3 Mkutano Mkuu utaitishwa na Katibu kwa kushauriana na
Mwenyekiti wa ngazi husika. Kamati tendaji
inaweza, kwa maombi kimaandishi, ya wajumbe wasiopungua theluthi moja ya
wajumbe wote. Kuitisha kikao cha Mkutano
Mkuu ikiona kuna haja na ulazima wa kufanya hivyo.
10.3.4 Taarifa ya
kikao cha Mkutano Mkuu itatolewa kwa wajumbe siyo chini ya miezi miwili kabla
ya kikao kwa taifa na mwezi mmoja kwa jimbo.
10.3.5 Endapo idadi ya
wajumbe waliohudhuria haifikii nusu ya wajumbe wa Mkutano, mkutano utahairishwa kwa muda usiopungua miezi
miwili. Lakini endapo mahudhurio ya wajumbe hao ni zaidi ya theluthi moja ya
idadi ya wajumbe wote wa Mkutano basi mkutano utafanyika.
11.0
WAJUMBE WA MIKUTANO YA
VIWAWA
11.1
TAIFA
11.1.1
Kamati Tendaji ya Taifa
11.1.2 Halmashauri ya Utekelezaji Taifa
11.1.2.1
Kamati Tendaji
11.1.2.2
Mwenyekiti wa kila Jimbo.
11.1.2.3 Mshauri kila Jimbo.
11.1.3 Mkutano Mkuu wa VIWAWA.
11.1.3.1 Kamati Tendaji ya Taifa.
11.1.3.2
Mwenyekiti, Katibu na Mhazini kila Jimbo
11.1.3.3
Mshauri,Mlezi wa Kila Jimbo
11.1.3.4
Mshauri wa Viwawa Taifa.
11.1.3.5
Wajumbe maalumu (Waalikwa) Ikiwa lazima.
11.2 KIJIMBO:
11.2.1 Kamati Tendaji ya Jimbo
11.2.2 Halmashauri ya Utekelezaji ya Jimbo.
11.2.2.1Kamati Tendaji ya Jimbo
11.2.2.2Mwenyekiti wa kila
Parokia.
11.2.2.3Mshauri wa kila Parokia.
11.2.2.4Mshauri wa Jimbo
11.2.3 Mkutano Mkuu wa
VIWAWA.
11.2.3.1
Kamati Tendaji ya Jimbo
11.2.3.2
Mwenyekiti, Katibu na Mhazini wa kila Parokia
11.2.3.3
Mshauri,Mlezi Jimbo.
11.2.3.4 Mshauri,Mlezi
kila Parokia
11.2.3.5
Wajumbe maalumu (Waalikwa) Ikiwa lazima.
11.3 KIPAROKIA
11.3.1 Kamati Tendaji Parokia
1.3.2 Halmashauri ya Utekelezaji Parokia
11.3.2.1
Kamati Tendaji
11.3.2.2
Mwenyekiti wa kila Kigango,Kanda,Jumuiya.
11.3.2.3
Mshauri Parokia
11.3.3.0 Mkutano Mkuu wa VIWAWA
11.3.3.1 Kamati ya Utendaji ya Parokia
11.3.3.2
Mwenyekiti, Katibu na Mhazini kila Kigango,Kanda,Jumuiya.
11.3.3.3
Mshauri,Mlezi wa Parokia..
11.3.3.4Wajumbe
maalumu.(waalikwa) Ikiwa lazima.
11.4.0 KIGANGO, KANDA
11.4.1 Kamati Tendaji ya Kigango,Kanda.
11.4.2.Halmashauri ya Utekelezaji ya Kigango,Kanda
11.4.3 Kamati Tendaji
11.4.4 Mwenyekiti,Katibu na
Mhazini kila Mtaa,Jumuiya.
11.4.5 Mshauri,Mlezi
Kigango,Kanda.
11.5.5 Mkutano Mkuu
11.5.5.1 Kamati Tendaji ya Kigango,Kanda.
11.5.5.2
Wanachama wote wa Kigango,Kanda,Jumuiya.
11.5.5.3
Mshauri,Mlezi wa Kigango,Kanda.
12.0 MAJUKUMU YA KAMATI
12.1 Majukumu ya Kamati Tendaji (Kigango, Parokia,
Jimbo na Taifa)
12.1.1 Kuhakikisha kuwa maazimio
ya chama yanatekelezwa
12.1.2 Kutayarisha hija, Semina,
Mafungo na Mikutano ya Chama.
12.1.3 Kudumisha uhusiano na
vyama vingine ndani na nje ya Kanisa.
12.1.4 Kutayarisha na kupanga
miradi mbalimbali kwa jumla.
12.1.5 Kuteua kiongozi atakayeshika nafasi
yoyote iliyo wazi hadi uchaguzi mkuu.
12.1.6 Kuteuwa wajumbe wa Kamati
Tendaji na Kamati ndogondogo za Chama.
12.1.7
Kutayarisha
Kalenda ya Matukio ya Mwaka.
12.1.8
Kuhakikisha
Katiba na Kanuni zinafuatwa na Kulindwa.
12.1.9
Kumwajiri Mratibu
na watumishi wengine wa viwawa.
12.1.10Kuitisha mikutano kwa mujibu wa Katiba.
12.1.11Kutoa Taarifa za Utendaji
katika mikutano.
12.1.12Kumsimamisha kiongozi,waajiriwa
walioshindwa kutekeleza majukumu na maadili ya chama.
12.1.13Kuhudhuria vikao,
mikutano, warsha, makongamano, ndani na nje ya chama.
12.1.14Kupokea, kujadili na
kuthibitisha taarifa za kamati ndogondogo.
12.2Majukumu ya
Halmashauri ya Utekelezaji (Kigango, Parokia, Jimbo, Taifa)
12.2.1 Kupokea, kujadili na
kupitisha taarifa za utekelezaji kutoka kwenye kamati tendaji na kuziwasilisha
katika mkutano mkuu.
12.2.2 Kupokea na kujadili hatua
za kinidhamu zilivyopendekezwa na Kamati Tendaji ili kuidhinisha na kutoa
mapendekezo kwa ajili ya kuwasilishwa kwenye mkutano mkuu.
12. 3 Majukumu ya Mkutano Mkuu (Kigango, Parokia, Jimbo
na Taifa)
12.3.1 Ni kikao cha juu kuliko vyote ya maamuzi ya
mwisho kuhusu mambo yote ya VIWAWA.
12.3.2 Kupokea na kujadili taarifa ya Halmashauri ya
utekelezaji
12.3.3 Kuchagua Viongozi wa Kamati Tendaji.
12.3.4 Kujadili na kupitisha makisio na ripoti ya
mapato na matumizi ya viwawa
12.3.5 Kuweka Maazimio.
12.3.6 Kuchunguza Muundo wa Chama.
12.3.7 Kupitisha marekebisho ya Katiba (ngazi ya
Taifa).
12.3.8 Kuchukua hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kumvua madaraka
Kiongozi yeyote wa viwawa au
kufuta uanachama wa mwanachama yeyote.
12.3.9 Kurekebisha, kusahihisha, kubatilisha uamuzi
wowote uliotolewa na vyombo vya chini yake.
13.0 MAPATO YA CHAMA.
13.1 Vyanzo vya mapato
13.1.1 Ada ya Uanachama. Kila
Parokia na Jimbo linapaswa kulipa ada kwa kiwango kilichokubaliwa kwa mwaka ili
kuchangia uendeshaji wa shughuli za viwawa katika ngazi zote.
13.1.2
Washirika
wahisani kutoka sehemu mbalimbali.
13.1.3
Shughuli za
kutunisha mfuko
13.1.4 Miradi
mbalimbali ya VIWAWA.
13.2
Uwekaji wa fedha
13.2.1 Fedha ni Lazima ziwekwe
Benki kwa jina la Chama.
13.3
Utoaji wa fedha
13.3.1 Ni lazima uwe na jina na
sahihi ya mweka hazina, mwenyekiti pamoja na mshauri wa chama.
13.3.2 Matumizi yote yapate
kibali cha kamati ya utendaji na mshauri.
13.4 Ukaguzi wa
fedha
Vitabu vya fedha na mali zote za chama zitakaguliwa kama ifuatavyo:
13.4.1 Taifa - Mkaguzi kutoka Taifa.
13.4.2 Jimbo - Mkaguzi wa Jimbo
13.4.3 Parokia - Mkaguzi wa Parokia
14.0 KAMATI NDOGO NDOGO
Kamati ndogondogo zinaweza
kuundwa kadiri ya mahitaji. Zifuatazo ni lazima ziwepo katika kamati tendaji.
14.1 Kamati ya Litrujia, Elimu na Mafunzo.
14.2 Kamati ya Michezo, Burudani na Mahusiano.
14.3 Kamati ya Uchumi, Mipango na Fedha .
14.4 Wajumbe wa Kamati:(ndogondogo)
Wajumbe wa kamati huteuliwa na
Kamati Tendaji kwa kuzingatia karama ya utume waliyonayo katika kamati husika na uwajibikaji
wake katika shughuli za kujitolea kwa kumtangaza Kristu kupitia karama
alizozawadiwa na Mungu, wajumbe wanne kutoka Halmashauri husika. Viongozi wa
Kamati Tendaji watakuwa wajumbe katika kamati hizo.
14.5 Majukumu ya
kamati ya Uchumi, Mipango na Fedha
14.5.1 Kuangalia na kusimamia miradi ya Viwawa katika ngazi husika.
14.5.2 Kubuni mbinu mpya ya kupata fedha za kuendesha
shughuli za chama, na kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya namna ya kutunza
hesabu.
14.5.3 Kubuni miradi mbalimbali, kupendekeza bajeti ya chama na kubuni
mbinu za kudhibiti matumizi.
14.5.4 Kutoa
taarifa ya maandishi kuhusu mapendekezo ya vikao vya Kamati kwa Kamati Tendaji, watakutana mara 1 kwa mwezi na
kwa dharula.
14.5.5 Kuhakikisha kila mjumbe wa kamati anapata haki ya kutoa mapendekezo
na ushauri ndani ya vikao.
14.5.6 Kushirikiana na Kamati
Tendaji na kamati zingine ndogondogo ili kuleta ufanisi katika kutekeleza
majukumu yaliyopo kwa wakati huo.
14.5.7 Kushirikiana na mhazini katika kutengeneza
repoti ya fedha ya mwaka.
14.6 Majukumu
ya kamati ya Litrujia, Elimu na Mafunzo
14.6.1 Kusimamia ibada za misa za vijana na
kuhakikisha huduma za Misa zimeandaliwa na kutoa taratibu za Misa.
14.6.2 Kusimamia malezi ya wanachama kwa njia za
mafundisho mbalimbali kama Biblia Takatifu, Tafakari ya Maisha.
14.6.3 Kuongoza na kuratibu ufundishaji wa sala na
tafakari ya Neno la Mungu na ibada mbalimbali zinazoongozwa na Viwawa.
14.6.4 Kuandaa Semina, Mafungo, Matendo ya Huruma,
Hija,Kongamano kwa vijana.
14.6.5 Kuhakikisha kila mjumbe wa kamati anapata haki
ya kutoa mapendekezo na ushauri ndani ya vikao.
14.6.6 Kutoa taarifa ya maandishi kuhusu mapendekezo
ya vikao vya kamati kwa Kamati Tendaji, na watakutana mara moja kwa mwezi na
kwa dharura.
14.6.7 Kushirikiana na na Kamati ya Utendaji. Kamati
zingine ndogondogo ili kuleta ufanisi katika kutekeleza majukumu yaliyopo kwa
wakati huo.
14.7 Majukumu ya Kamati ya
Michezo, Burudani na Mahusiano
14.7.1 Kusimamia michezo na
kupanga michezo mbalimbali ya chama kama mpira wa
miguu,mpira wa
kikapu,mpira wa pete.
14.7.2 Kuandaa michezo na mashindano mbalimbali kwa
kushirikiana na viongozi wa Kamati
Tendaji.
14.7.3 Kuanzisha timu za michezo ya nje mfano mpira
wa miguu, kikapu, na pete
14.7.4 Kuandaa michezo ya kuigiza mfano Mateso ya
Yesu, Fatima, Bakhita na mingine itakayojitokeza.
14.7.5 Kuanzisha vikundi vya utamadunisho mfano
ngoma, Ngonjera, Jaiving, nyimbo.
14.7.6 Kuandaa na kuratibu sherehe na burudani
mbalimbali ambazo chama zitakuwa nazo katika kipindi cha mwaka mfano pikiniki,
sherehe.
14.7.7 Kutoa taarifa za maandishi kuhusu mapendekezo
ya vikao vya kamati kwa Kamati Tendaji, watakutana mara moja kwa mwezi na kwa
dharula.
14.7.8 Kuhakikisha kila mjumbe wa kamati anapata haki
ya kutoa mapendekezo na ushauri ndani ya vikao.
14.7.9 Kushirikiana na Kamati ya Utendaji.Kamati
zingine ndogondogo ili kuleta ufanisi katika kutekeleza majukumu yaliyopo kwa
wakati huo.
mnaweza kunitumia pdf
ReplyDeleteAsante sana kwa Elimu mungu akubariki
ReplyDeleteNaomba PDF mtumishi
ReplyDeletePdf please tunahitaji ni mhimu kwa vijana
ReplyDeleteAsante Swali langu je kiongoz ngazi kuu viwawa kamat tendaji akiwajibishwa kwa mujibu wa kanuni kwa utovu wanidham ikiwepo utatatishaji fedha za vijana anaruhusiwa kuchaguliwa tena kuwa kiongoz kandaa??
ReplyDeleteMapendooooo, sioni sehemu ya ku download pdffff
ReplyDeleteMnaweza nitumia whatsapp 0623056162
ReplyDeleteMe pia sioni sehemu ya kudownload kama mnawez naomb mtumie kwa whatsap namba 0754929091
ReplyDelete