USHIRIKA WA VIWAWA NI NINI?
Viwawa ni ushirika mkubwa wa
vijana ambao kwa matendo na tafakari hujaribu kubadii na kukuza/kustawisha
maisha yao nay a jamii.
VIWAWA: ni chama cha kitume cha Vijana Wakatoliki Wafanyakazi
ambao wanatumwa na Kanisa ili neza habari njema ya kwamba Yesu Kristu ndiye
njia ya ukweli na uzima kwa vijana wote katika maisha yao ya kila siku.
Wafanyakazi: Ni vijana wa wanaume na wanawake waishio mijini, vijijini
na walio kwenye masomo, mafunzo ya fani mbalimbali, walio katika ajira rasmi na zisizo rasmi.
Viwawa ni chama ambacho kinawaunganisha vijana na
kuwasaidia waone hali yao, kuamua juu yake katika mwanga wa Injili na
kuwaongoza kufanya matendo ya kubadilisha hali zao na kutengeneza ziwe nzuri
zaidi kwa njia ya Tafakari ya Maisha.
Chama hiki huongozwa na vijana wenyewe katika ngazi zote
na huwa na Mshauri na Mlezi kwa ngazi ya Parokia,Jimbo na Taifa.Soma zaidi
katiba ya viwawa Tanzania
NANI ANAENDESHA VIWAWA?
Viwawa inaendeshwa katika ngazi ya jumuiya, vigango,
parokia,majimbo taifa na kimataifa na vijana wenye umri kati ya miaka 14 mpaka
35. Vijana huamua mambo ya kufanya baada
ya kutathimini uhalisi wa mazingira, pamoja na hali ya watu wanaowazunguka.
VIWAWA INAFANYA SHUGHULI GANI?
Viwawa huwakusanya vijana pamoja na kuwasaidia kupata majibu
ya mahitaji yao na mahitaji ya vijana wengine kupitia matendo.matendo haya
huamuliwa katika vikundi kupitia majadiliano yajulikanayo kama DODOSO(njia ya
kushirikishana matatizo na changamoto zinazowakabili)
Matendo yanaweza kufanywa na mwanachama mmojammoja kwa
kuwasaidia marafiki kutatua matatizo katika kazi zao, familia na mahusiano.
Matendo ya viwawa pia hufanywa na vijana kwa pamoja katika vikundi.
Mfano:
·
Kufanya kampeni juu ya haki za vijana
·
Kufanya kazi ili kupata zana bora
·
Kuandaa matukio ya kuwasaidia vijana wasiojiweza
Kwa njia hii viwawa inaweza
kusaidia maendeleo ya jumuiya.
KITU GANI KIZURI ZAIDI KUHUSU
VIWAWA?
Zaidi ya ukweli kuwa viwawa
inaendeshwa na vijana wenyewe, inasababu nyingine tatu muhimu za kuwepo.
1.
Ni nafasi ya kuitumia kuchukua hatua kuboresha
jamii ndogondogo na jamii kubwa
2.
Viwawa wanasaidia kujenga ujasiri, ujuzi
binafsi, imani, kujitambua kwa vijana.
3.
Viwawa wanasaidia vijana kukutana na marafiki
wapya nchini kote na hata duniani kote kupitia matendo yao, mikutano katika mafunzo,
likizo na mikusanyiko mbalimbali.viwawa ni uzoefu wa thamani inayofurahisha.
VIWAWA ILIANZAJE?
Viwawa ilianzishwa Ubelgiji mwaka wa 1925 katika jumuiya ya
wafanyakazi waliokuwa wakiishi nje kidogo na mji wa Brussels na Padri kijana
aliyeitwa Joseph Cardijin.Padre Cardjin alijihisi kutengwa na marafiki zake kwa
kuamua kuwa padre na alikuwa anaguswa na jinsi ya wafanyakazi walivyokuwa
wanawekwa mbali na kanisa.Aliamini kuwa ujumbe wa Yesu ulikuwa kwa ajili ya
wafanyakazi na maskini, na hivyo alijitoa katika kuwaunganisha kwa ajili ya
kazi ya tafakari ya Injili na matendo ya jamii.
KWA JINSI GANI USHIRIKA WA VIWAWA UNA UMUHIMU LEO?
Viwawa inapatikana katika nchi zaidi ya 100 ulimwenguni kote
na ina wanachama zaidi ya milioni 3. Kwa zaidi ya miaka 70 iliyopita, viwawa
ilikuwa na msukumo endelevu wa mabadiliko kama ambavyo imekuwa ikipanuka
ulimwenguni kote.
NITAJIUNGAJE NA VIWAWA?
Kuna vikundi vidogo vidogo katika ngazi ya Parokia
nchini kote. Vikundi hivyo hukutana mara
kwa mara kupanga mambo ili kuwahudumia, kuwaelimisha na kuwawakilisha vijana.
Ili uweze kujinunga wasiliana na viwawa kwa kutumia anuani iliyoko nyuma ya
kipeperushi hiki na watakueleza wapi kikundi cha karibu kinapatikana.
Vinginevyo waweza
kumuuliza Paroko wa Parokia yako au kiongozi wa kanisa. Hakika viwawa ni uzoefu
wa thamani inayofurahisha.
NINAHITAJI KUCHANGIA FEDHA?
Ndio, kila kijana hulipa kiasi kidogo cha ada kwa viwawa kwa
ajili ya kujiunga pamoja na michango ya kikundi Parokiani.Kwa kupitia
uwajibikaji huu, wanachama watajishughulisha na hivyo kumiliki ushirika wao
wenyewe.
VIWAWA NI KWA AJILI YA NANI?
Ni kwa ajili ya kila mmoja.Kila kijana mwenye umri kati ya
miaka 14 hadi 35 anaweza kuwa mwanachama. Wale wenye umri wa miaka 14 -17 huwekwa pamoja( hawa ni wale
ambao bado wanasoma muda wote au wanasoma kwa muda mfupi katika ufundi stadi).
Uanachama wa kudumu kwa miaka 18 na kuendelea uko wazi kwa waliomaliza masomo,
wafanyakazi wakudumu au wa muda, wazazi au wanaotafuta kazi.viwawa inahusika
kwa namna ya pekee na kundi la vijana wafanyakazi katika jamii ya kisasa.
USHIRIKA HUU UNAENDESHWAJE?
Viwawa ina ngazi mbalimbali katika uendeshaji, ngazi ya
mwanzo nay a muhimu ni ngazi Jumuiya, Kufuatiwa na vigango na Parokia na
hujumuisha vijana ambao hukutana jumuiyani pamoja na kuchagua viongozi wao,
huchangia mfuko wao wa fedha na kuamua matendo kulingana na mahitaji
yanayowazunguka. Viwawa pia ina ngazi za
jimbo, taifa na kimataifa ili kusaidia na kukuza kazi za jumuiya,vigango na
parokia.wawakilishi wao waliochaguliwa hupeleka maoni katika ngazi hizi na
husaidia katika malezi na mafunzo ya uongozi wa shirika.
KWA NINI VIWAWA INAITWA SHULE YA MAISHA?
Viwawa ni shule ya maisha kwa sababu sio tu huzungazitia
vijana wa leo bali pia hukuza ujuzi wao wa kuwasiliana na kujiendesha ambao huwafaa
kama viongozi. Malezi yao haya huzaa viongozi sio tu kwa ajili ya ushirika huu
lakini pia kwa maisha yote.Hivyo hutoa mchango ulio wazi katika kanisa na
katika jamii.
NI KWA VIPI VIWAWA NI USHIRIKA WA KIKRISTU?
Viwawa inaongozwa na mafundisho ya Kristo, kazi yake
inaongozwa na tafakari ya Injili ambayo huwa ndiyo utangulizi msingi wa kila
mkutano. Hii huthibitisha hadhi na lengo ambavyo Mungu amempatia kila kijana
kwa maisha.Misingi ya mwanzo ya ushirika huu ni Padre Cardjin na Kanisa
Katoliki; vile vile hutafuta namna ya kushirikishana na madhehebu mengine,
ukiamini kuwa taratibu na malengo yake yatapokelewa na madhehebu yote.
JE WATU WAZIMA HUSHIRIKI KATIKA VIWAWA?
Ndio, zaidi ya viongozi wa kuchaguliwa katika jumuiya, pia
kuna mlezi/mshauri. Kwa kawaida huwa ni Padre ingawaje hata sasa anaweza kuwa
Mlei, Mtawa,au Katekista.Kazi ya Mlezi/Mshauri ni muhimu sana kwa malezi ya
vijana, lakini hasa katika kuwaunga mkono na kuwasaidia na si katika kuongoza.
Ushirika huu una muundo wake wa kujitegemeza na hutoa
mafunzo kwa ajili ya walezi/washauri wake.
Asante sana, Mungu akubariki
ReplyDeleteahsante nitumiwe
ReplyDeleteahsante nitumiwe
ReplyDeleteNashukuru
ReplyDeleteUmeeleweka Ameeeeen
ReplyDeleteNi ujumbe mzuri na elimu tosha kwa vijana wote.
ReplyDeleteUbarikiwe Sana.
Shukrani sana nimeelewa
ReplyDeletePongezi kwa waandaaji, kupitia maelezo haya vijana wataamasika zaidi kujiunga na viwawa Parokiani hii ni elimu tosha.
ReplyDeleteAsante sana
ReplyDeleteNashukuru kwa elimu uliyotupatia nimefurahi
ReplyDelete